Karibuni sana wasomaji wetu wa tovuti hii ambayo ni maalumu
kabisa kwa kupanua wigo wa kuielewa biblia ilivyo na uhalisia unaoendelea
katika dunia hii.Hii ni makala ya kwanza kabisa kwa wasomaji wetu wa tovuti hii katika mfululizo wa matoleo
yatakayo endelea.Kwa kuwa yanayoandikwa humu
ni mambo yaliopo kwenye biblia na kwa kuwa wasomaji wa makala hii ni
wasomaji wa biblia hiyohiyo, sitaki kumaanisha ninawakwaza watu kwa kuidadisi
biblia,bali ni sehemu ya kupata changamoto, elimu na kukumbushana kuisoma
biblia na kuielewa.Pia ninazitambua juhudi za waandishi wa biblia kuchangia
kueneza neno la mungu ambalo tunalo sasa na kuliishi wamefanya kazi kubwa
sana.Bila kuwasahau wahubiri wetu wa neno la mungu maaskofu, mapadre wachungaji
mbalimbali na wazee wa makanisa mbalimbali duniani kwote wamefanya na wanafanya
kazi kubwa ya kueneza injili kwetu natambua mchango wao ambao umeifanya dunia
kuwa tulivu ,na watu kuwa wastaarabu na kuwa na ujuzi mbalimbali wa kiroho na
hata wa kiuchumi,utamaduni na kisiasa kwenye jamii zetu.Mimi si wa kwanza
kuidadisi biblia na kufikia hatua ya kusema siiamini biblia bali wapo wengi tu
duniani labda huenda hatujaielewa bado kuwa inamaanisha nini mpaka sasa.Nipo
tayari kuamini uhalisia wowote unaoendana na maandiko.Nipo tayari vilevile
kupokea ushahidi wa maandiko ya biblia na uhalisia uliopo sasa
unaoendelea.Simzuii mtu kutoa maoni yake ila yaendane na maandiko ya
biblia.Sikatai ushauri kutoka kwa yeyote Yule ijapokuwa wapo watakaopingana na hoja
nitakazoziweka hapo chini.Haitakuwa busara kutoa lugha za matusi au lugha
zinazofanana na matusi kwa sababu lengo kubwa ni kupeana elimu juu ya biblia
kutokana na mfululizo wa hoja nilizonazo na ambazo zipo kwenye biblia
hiyohiyo.Kinyume na hapo utakuwa unagombana na biblia yenyewe.
Nimekuwa nikiiamini biblia na bado ninaifurahia kama fasihi
(huenda siisomi au ninaisoma sana kuliko wengi marafiki wakristu wenzangu)
lakini siitumaini kama ni kitabu chenye nguvu ya kimungu kwa mtazamo wa
kibinadamu tulionao. Kwa nini? Majibu ni marefu sana na ni magumu kidogo hivyo
sitakuchosha sana wewe msomaji wa makala hii.
“BIBLIA ni neno la MUNGU”.Hili wazo tunalo na tunaishi nalo
kila siku.Tena tunaenda mbali na kusema “MUNGU aliandika biblia”.Na tukiendelea
tukisema “KITABU CHA MUNGU”Huu ni ufahamu wa hali ya juu na utaalamu wa kuwapa
watu moyo,matumaini na faraja kipindi cha taabu nyingi wakati wa kukabiliana na
mambo yasiyojulikana.Wakristu,wayahudi,waislamu,wamomoni,wahindu,wabudha na
wengineo ambao wanadai kuwa na maandiko yenye nguvu za kimungu wanashuhudia
haya kila siku.
Jambo hili nikajikuta nashindwa kulikalia kimya.Na
ninajikuta ninachagua njia niliyonayo sasa ya kutokuwa na imani na biblia kama
ni neno la mungu.Na nitashangaa kama shetani ndiye aliyenidanganya kuyasema
haya au la.
Tunaposoma biblia maranyingi tunakuwa na mawazo kati ya haya
mawili:
(i)Biblia inapumzi ya mungu angalau kwa kiasi Fulani
(ii)Biblia imeandikwa na binadamu tu kwa utashi wake bila
nguvu ya mungu ndani yake
Ninavyoona mimi kwamba kama mtu akichunguza biblia kwa
usahihi,atachagua namba mbili
(a)Biblia imesheheni kauli nyingi sana ambazo zinapingana
zenyewe kwa zenyewe na zinatatiza
Ilishawahitokea kwamba niliwahi kutaka hadharani kuwa biblia
ni sahihi,inamsimamo , haidanganyi na haina utata hata kama imeandikwa na
waandisho zaidi ya 40 na hata kama imeandikwa zaidi ya miaka 1500.Inasimulia habari moja moja na
ni zilezile na ndio utamaduni wa kikristu ambao umeingia kwenye utamaduni wa
kiprotestant uliokithiri kwa sasa.Kuna wachambuzi mbalimbali wa biblia akiwemo
huyu kutoka ISRAEL (UYAHUDI) anaitwa :
MICHAEL KARASIK anasema “Sehemu mbalimbali za biblia
zimeandikwa vipindi tofauti,kwa mtindo tofauti na watu tofauti wenyemitazamo
tofauti.Na kwamba dunia ni kama yetu tu ilikuwepo na watu walitofautiana kwa
kelele nyingi maranyingi kuhusu siasa,na kuhusu dini.Tofauti hizi pamoja na
zingine ambazo wakati mwingine za binafsi sana ndio zote zinazopatikana leo
zilizokusanywa na ndizo tunazoziita biblia”
Huyu ni msomi wa kiyahudi wa biblia.
Mwingine ni JAQUES
BERLINABLAU ambaye ni mwandishi wa fasihi ya wahebrania wa kale anasema kama
ifuatavyo “Miongoni mwa changamoto
kubwa sana ambazo mhadhiri wa biblia chuoni anakabiliana nazo ni kudhaniwa
kutofikiri kuwa biblia ni kitabu cha kisasa.
Wengine ni wachambuzi wa vitabu vya deuterokanoni ambao ni
Profesa Ronald J. Alen na Joseph katika kitabu chao wanasema “injili moja
masikio mengi”waandishi wa biblia wanatofautiana.
Kwa mfano wadeuterokanoni
wana wanachukulia kwamba utiifu unazaa ustawi na mafanikio wakati jeuri inakaribisha laana.Lakini kitabu cha AYUBU
kinasema kwamba “sio lazima”
Wasomaji wanashauriwa kwenye kitabu cha 1 PETRO kwamba kuwa watiifu kwa watawala kwa kuwa
watawala ni wawakilishi wa mungu.Lakini kitabu cha ufunuo kinatazama kama dola
ya kirumi ni kifaa cha shetani.....itaendelea toleo lijalo.
Comments